Tunakupa unachohitaji sasa na baadae

Propellerads
  • WELCOME TO Adonisstunner Blog FOR UPDATED NEWS AND ENTERTAINMENTS

    Search

    Jumapili, 26 Februari 2017

    AJALI MBAYA LUSHOTO, SITA WAFARIKI ,SABA MAJERUHI,,,,

    Watu sita (06)  wamepoteza maisha na wengine saba kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wamepanda aina ya Canter lenye namba za usajili T 634 ADF lililokuwa likitokea mnadani Mlalo kwenda Soni.

    Gari hilo lilipata ajali baada kuacha njia na kupinduka katika kijiji cha Mgaro Kata ya Mgaro Tarafa ya Mlalo wilayani Lushoto.

    Waliofariki katika ajali hiyo kwa mujibu wa kamanda ni Jamali Hemedi, Khadija Saidi, Zuena Juma, Husna Athumani, Nusura Seif na Hassan Rashid.

    Aidha, waliojeruhiwa wametajwa kuwa ni Seif Bakari, Sauda Shemtui, Mwanahamis Ayoub, Abeid Ayoub, Khalifa Juma, Mariam Kassim na Mwanamvua Yusuph.

    Kamishna Mwandamizi wa Polisi, Benedict Wakulyamba ambaye ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo, na ameeleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva kupita kwenye mlima mkali wenye utelezi ulionyeshewa mvua.




    Hakuna maoni:

    Chapisha Maoni

    Search

    Chapisho Lililoangaziwa

    NEW HIT:OMMY DIMPOZ FT ALIKIBA-KAJIANDAE

    Toa Maoni yako

    Jina

    Barua pepe *

    Ujumbe *

    Wanaofuata

    Propellerads